Reader ready.
Brief Presentation on Islam (Article - Swahili)
This is an article in Swahili gives a brief presentation on Islam.
Contributors
AuthorsScientific Research Admission of Islamic University , Madinah Munawara
Sourcesiu - The Islamic University Website in Almadinah Almunawara
Download all material files
2 files • 1.5 MB
Material files
1 / 2Social-friendly share text
Nitafurahi kushiriki hili nawe:
📄 MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU UISLAMU (Kiswahili)
📝 Ama baada:_ NUKTA YA KWANZA: NGUZO ZA IMANI NGUZO YA KWANZA:- NI KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU MMOJA. NGUZO YA PILI:- KUAMINI MALAIKA NGUZO YA TATU:-KUAMINI VITABU A-TAURATI: B- INJILI: C- ZABURI: D- NYARAKA: E- QURANI TUKUFU:- NGUZO YA TANO:KUAMINI SIKU YA MWISHO. NUKTA YA PILI: NGUZO ZA UISLAMU NGUZO YA KWANZA: SHAHADA MBILI. NGUZO YA PILI: SALA NGUZO YA TATU: ZAKA NGUZO YA NNE:SAUMU NGUZO YA TANO:-HIJA Miongoni mwa hizo ibada tukufu ni:- NUKTA YA TATU:IHSAN Na kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu المملكة العربية السعودية وزارة التعليم العالي الجامعة الإسلامية بالمدينة المنورة عمادة البحث العلمي قسم الترجمة تعريف موجز بالإسلام (بللغة السواحلية) بسم الله الرحمن الرحيم MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU UISLAMU Kila sifa njema ni zake Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe vyote, sala na amani ziwe juu ya Imamu wa Mitume, Nabii wetu Muhammad, na jamaa zake, na Masahaba wake wote. Ama baada:_ UISLAMU:_ ni kushuhudia kuwa hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu mmoja, na Muhammad (rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu, (kushuhudia) kwa moyo, na kwa ulimi, na kwa viungo. Na (huo Uislamu) unajumuisha kuamini nguzo sita za Imani kwa kutekeleza nguzo tano za Uislamu, na nguzo mbili za Ihsani. Na (huo Uislamu) ni risala ya mwisho miongoni mwa risala za Mwenyezi Mungu, ambayo ameiteremsha Mwenyewe Allah kwa mwisho wa manabii wake na mitume wake, Mtume Muhammad bin Abdillah (rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) . Na (huo Uislamu) ndiyo dini ya haki ambayo Mwenyezi Mungu hatakubali dini nyingine isiyokuwa uislamu, na hakika ameifanya Mwenyezi Mungu dini ya uislamu kuwa nyepesi na rahisi, hakuna ugumu au uzito ndani yake, wala tabu, hakuwalazimisha (Allah) wenye kuingia ndani ya dini hiyo mambo wasiyo yaweza, na wala hakuwakalifisha kwa yale wasiyoweza. Na ni dini ambayo msingi wake ni TAUHID (kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika ibada) , na alama yake ni ukweli, na imezungukwa na uadilifu, na ndiyo usimamizi wa haki, na roho yake (dini hii) ni huruma, na ni dini tukufu ambayo huwaongoza waja (watu) kwenye kila jambo lenye manufaa katika dini yao na dunia yao, na huwatahadharisha kutokana na kila lenye madhara katika dini yao na maisha yao, Na ni dini ambayo Mwenyezi Mungu amerekebisha kwayo itikadi na tabia, na akarekebisha kwayo maisha ya duniani na Akhera, na akaziunganisha kwayo nyoyo zilizo tafautiana, na matamanio mbali mbali, akazisafisha kutokana na sifa za upotofu, na akazielekeza kwenye haki, na akaziongoza kwenye njia iliyo nyooka. Na ni dini iliyo sawa iliyo kamilika isiyokuwa na kasoro katika habari zake zote, na hukumu zake zote, haikuelezea ila ukweli na haki, na wala haikuhukumu ila kwa kheri na uadilifu, miongoni mwa itikadi sahihi, na vitendo vilivyo sawa, na tabia bora, na desturi za hali ya juu. Na ujumbe wa Uislamu unalengo la kutimiza mambo yafuatayo: ~ Kuwajulisha watu mola wao na muumba wao kwa majina yake mazuri ambayo hakuna mwenye majina hayo isipokuwa yeye tu, na sifa zake za hali ya juu ambazo hakuna mwenye kufanana nae katika sifa hizo, na vitendo vyake vya hekima ambavyo hana mshirika kwenye vitendo hivyo, na kustahiki kwake (majina hayo, na sifa hzo, na vitendo hivyo) ambako hana mshirika ndani yake. ~ Kuwalingania waja (watu) ili wamuabudu Mwenyezi Mungu pekeyake hana mshirika, kwa kufuata mambo aliyo wawekea sheria katika kitabu chake (Qurani) na Sunna za mtume wake (Muhammad rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake) miongoni mwa maamrisho, na makatazo ambayo ndani yake mna kutengenea kwao katika dini yao, na akhera yao. ~ Kuwakumbusha hali yao na marejeo yao baada ya kufa na mambo watakayo kutana nayo ndani ya makaburi yao, na wakati wa kufufuliwa kwao , na kuhesabiwa kwao, na mwisho wao ima peponi au motoni. Mwenyezi Mungu atawalipa kulingana na matendo yao, aliye tenda wema atalipwa wema, na aliye tenda uovu atalipwa uovu. Na tunaweza kufupisha misingi muhimu ya Uislamu kwenye nukta zifuatazo:- NUKTA YA KWANZA: NGUZO ZA IMANI NGUZO Y...
🔗 https://b.islamhouse.com/sw/articles/435